Wednesday 24th April 2024, 06:58 am

logo

The United Republic of Tanzania

CONTRACTORS REGISTRATION BOARD

  • crblogo

photo is coming soon MAKANDARASI wametakiwa kuacha kuomba zabuni kwa gharama za chini, ili kuwavutia watoaji wa kazi, kwa kuwa uzoefu unaonyesha wamekuwa wakishindwa kuzikamilisha na wengine kukimbia baada ya kuzipata. Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Morogoro na Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Mhandisi Consolata Ngimbwa wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa makandarasi wazalendo. Alisema baadhi ya makandarasi wamekuwa wakijaza hela ndogo kama mbinu ya kushinda zabuni lakini wanapopata kazi hizo wanashindwa kuzikamilisha kwa wakati na wengine kushindwa kuzikamilisha kabisa. “Jazeni zabuni vizuri tena kwa uhalisia msijaze tu ilimpate zabuni lakini mwishowe zinawashinda, hapa katikati tuliyumba sana baada ya serikali kuanza kufanyakazi zake kwa kutumia utaratibu wa force account sasa tumeanza kupata kazi za serikali tusifanye makosa, tuzifanye kwa weledi mkubwa,” alisema Ngimbwa. Alisema CRB iliamua kuanza kutoa mafunzo hayo kwa makandarasi baada ya lawama nyingi kwamba makandarasi hao wamekuwa wakiweka bei ambazo hazina uhalisia. Mhandisi Ngimbwa aliwasisitiza pia kufanyakazi kwa ubia na makandarasi wenzao na wanaposhindwa kujua namna ya kuzifanya wafike ofisi za bodi hiyo au kwa wataalamu kwaajili ya kuelekezwa namna ya kufanyakazi za aina hiyo. “Wengi tunaingia kwenye kazi za ubia lakini tunashindwa sijui kwasababu hatuzijui au, uzuri wa kazi hizi ni kwamba mnaunganisha nguvu na kufikia vigezo vinavyohitajika na kama mkishindwa njooni CRB mtaelekezwa,” alisema.
Photo by:Admin, 2021-08-17 12:29:05
photo is coming soon MAKANDARASI nchini wameelezwa kuwa matumizi ya mfumo wa manunuzi ya umma kielekroniki (TANePS) ni ya lazima kwao hivyo wanapaswa kuufahamu vyema na kuutumia kwaajili ya kuwasilisha zabuni zao mapema. Hayo yamesemwa mwishoni mwa wiki mkoani Morogoro na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB),Qs Joseph Tango, wakati wa mafunzo ya namna ya kutumia mfumo huo na wajibu wa mkandarasi. Tango alisema ni muhimu kwa makandarasi kufanya maandalizi ya zabuni mapema na kuziwasilisha kwa njia ya mfumo huo kama ni mradi wa serikali kwani tabia ya kufanya kwa mtindo wa zimamoto hauwezi kuleta matokeo mazuri. “Kwenu nyinyi ujuzi wa kutumia mfumo huu wa kielektroniki ni lazima kwasababu mwajiri mkubwa wa mkandarasi ni serikali na kwa sasa huwezi kushiriki zabuni ya kazi za serikali bila kupitia mfumo huu.” alisema “Na mjenge kawaida ya kufanya mapema kwani mfumo huu ni wa kielektroniki na chochote kinaweza kutokea na kukufanya uchelewe kuwasilisha zabuni kwa mfano hitilafu ya umeme mahali ulipo au udhaifu wa mtandao wa intaneti haya yote yatakukwamisha.” Alisema. Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Qs. Joseph Tango akifunga mafunzo ya siku tatu kuhusu wajibu wa makandarasi na namna ya kujaza zabuni kielektroniki yaliyoendeshwa na bodi hiyo mkoani Morogoro kwa siku tatu na kumalizika siku ya Ijumaa.
Photo by:Admin, 2021-08-17 11:37:57
photo is coming soon Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 19 Desemba, 2018 ameweka jiwe la msingi la upanuzi wa barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam katika sehemu ya kuanzia Kimara hadi Kibaha yenye urefu wa Kilometa 19.2. Upanuzi huo utahusisha kuongeza njia za magari kutoka 2 zilizopo sasa hadi 8, kujenga madaraja 6 na makalavati 36, na kujenga barabara ya juu (Flyover) katika eneo la Kibamba CCM kwenye makutano ya barabara inayotokea Bunju na barabara ya kwenda hospitali ya Mloganzila.
Photo by:Admin, 2020-05-05 16:56:33

Notice Board

Click "New" Icon Below To View Adverts

BUSINESS MASTERY TRAINING
DELETION OF CONTRACTORS
CONTRACTORS REVIEW INFORMATION FORM
EVENTS CALENDAR FOR THE FINANCIAL YEAR 2023/24
ONLINE PROJECT REGISTRATION MANUAL
PROCEDURE FOR CHANGING NAMES, SHAREHOLDERS AND DIRECTORS

Video Adverts

Photo Gallery

Subscribes For Newsletter