Thursday 1st May 2025, 04:45 am

logo

The United Republic of Tanzania

CONTRACTORS REGISTRATION BOARD

  • crblogo

From The Press

photos are coming soon Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi CRB Mhandisi Joseph Nyamhanga, amemtaka mkandarasi anayetekeleza mradi wa usambazaji wa umeme vijijini (REA) mkoa wa Manyara katika Wilaya ya Babati, Simanjiro na Kiteto, na kampuni ya China Railway Construction Electrification Bereau Group Company Limited (CRCEBG) kukamilisha mradi huo kwa wakati ili wananchi wapate huduma ya umeme. Amesema hayo tarehe 18 Februari mwaka huu katika ziara ya Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti ya CRB inayofanywa katika mikoa minne ya kanda ya kaskazini ambayo ni Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga kwa lengo la kukagua kazi za Makandarasi. Mhandisi Nyamhanga amesema kuwa hatua ya serikali kusambaza umeme katika kila kitongoji nchini imelenga kuhakikisha kila mwananchi anafikiwa na huduma ya umeme kwa gharama nafuu. Aidha msimamizi wa mradi Mhandisi Michael Masimbani amesema mradi huo umelenga kufikisha huduma ya nishati ya umeme katika kata 139 ambao thamani yake ni zaidi ya shilingi bilioni 21na miongoni mwa wanufaika ni pamoja na kitongoji cha Maisaka ambapo tayari nguzo zimeshasimikwa na nyaya zimeshavutwa na kwamba kilichosalia sasa ni ufungaji wa transfoma. Aidha ujumbe huo wa Bodi na Menejimenti CRB umetembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa makumbusho ya Hifadhi ya Ngorongoro wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 23 unaotekelezwa na Mkandarasi China Railway 25 Group Ltd katika Wilaya ya Ngorongoro. Akitoa taarifa kwa wajumbe hao wa Bodi ya CRB Mjeolojia Ramadhan Khatibu kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro amesema makumbusho hayo yanatarajiwa kukamilika mwezi mei mwaka huu ambapo itaongeza idadi ya watalii watakao tembelea katika hifadhi hiyo. Sambamba na hayo Bodi hiyo imetembelea mradi wa upanuzi wa maji wa kilometa 48 unaotoka tenki la maji la Ngorbob jijini Arusha unaotekelezwa na Mkandarasi Jandu Pumblers Ltd katika eneo la Nanja wilaya ya Monduli ambao umelenga kutatua changamoto ya maji kwa wakazi wa wilaya hiyo na vijiji vya jirani. Pamoja na hayo Mwenyekiti wa Bodi ya CRB Mhandisi Nyamhanga amemtaka Mkandarasi Jandu Plumbers kuhakikisha anakamilisha mradi huo kwa kwa ubora unaotakiwa kwa kuzingatia gharama halisi kwa mujibu wa mikataba yao ili kutimiza azma ya Serikali ya kufikisha huduma ya maji kwa wananchi kwa wakati.
Photo by:Admin, 2025-03-26 05:48:21
photos are coming soon Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), imesema inaanza operesheni maalum ya kukagua miradi mikubwa inayotekelezwa na Makandarasi kutoka nje ya nchi, kutokana na miradi mingi kutekelezwa chini ya viwango. Aidha imebaini hayo kufuatia ziara mbalimbali za Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa katika miradi mbalimbali ikiwemo barabara ambayo imeonekana kuwa na changamoto kubwa. Akizungumza leo jijini Arusha, katika ufunguzi wa mafunzo ya usimamizi wa fedha kwa Makandarasi,Msajili wa CRB, Rhoben Nkori, alisema Bodi hiyo imeamua kufanya operesheni hiyo maalum kuanzia mwezi Mei hadi katikati ya mwezi Juni mwaka huu. Aliwataka Makandarasi wote kutambua kuwa operesheni hiyo maalum itafanyika hadi mwezi Juni, 2024 ili kujiridhisha Makandarasi wote walioingia mkataba na serikali kama wanafanya kwa mujibu wa mikataba waliyoingia na sheria, kinyume na hapo hatua zitachukuliwa. “Bodi iemamua kufanya operesheni maalum ya kutembelea miradi na kukagua miradi yote mikubwa inayofanywa na wakandarasi wa nje kwasababu miradi mingi mikubwa inafanywa na wakandarasi wa nje,”alisema.
Photo by:Admin, 2024-05-16 06:26:32
photos are coming soon Waziri wa Ujenzi, innocent Bashungwa ameziagiza Bodi za Usajili wa Makandarasi (CRB) na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), kuhakikisha zinaandaa mpango kazi wa kusimamia na kuimarisha taaluma ya Sekta ya Ujenzi nchini ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo wataalamu wake ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya Teknolojia. Bashungwa ameyasemaa hayo leo Tarehe 06 Novemba, 2023 jijini Dodoma, alipokuwa akizindua Bodi za ushauri za CRB na ERB ambazo zinaundwa kwa mujibu wa sheria ili kusimamia utekelezaji wa majukumu ya Bodi hizo. Amesema kuwa Takwimu zinaonyesha kuwa suala la upatikanaji wa fursa nchini katika utekelezaji wa miradi kwa makandarasi wa ndani haliridhishi kutokana na kuwa licha ya makandarasi wa ndani kuwa wengi bado miradi wanayoitekeleza ni michache ukilinganisha na makandarasi wa nje. “Muandae mpango kazi wa kusaidia Makandarasi wa ndani, muujadili, kuutathmini na kuusimamia kwa pamoja badala ya kulalamika makandarasi wa ndani hawapati fursa”, amesema Bashungwa. Pia, Bashungwa amesisitiza kwa bodi hizo kuongeza ushirikiano mzuri walionao ili kusaidia taaluma hiyo kufanya kazi vizuri na kuleta maendeleo nchini.
Photo by:Admin, 2023-11-07 06:02:40

Notice Board

Click "New" Icon Below To View Adverts

PROCEDURE FOR CHANGING NAMES, SHAREHOLDERS AND DIRECTORS

Video Adverts

Photo Gallery

Subscribes For Newsletter