Tuesday 3rd October 2023, 12:58 pm

logo

The United Republic of Tanzania

CONTRACTORS REGISTRATION BOARD

  • crblogo

From The Press

photos are coming soon Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, ameagiza Wizara kupitia Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), kuhakikisha wanakuja na mikakati ya kuwawezesha Makandarasi Wazawa kushirki katika Utekelezaji wa miradi ya Sekta ya Ujenzi nchini ili kuleta tija kwa Makandarasi hao na Taifa kwa ujumla. Ameyasema hayo Septemba 26, 2023 jijini Dodoma, wakati alipokutana na kupokea taarifa za utekelezaji wa majukumu ya Taasisi za Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC). Bashungwa ameagiza Wizara kukaa na kusikiliza changamoto zao na kuzitafutia ufumbuzi pamoja na kuandaa mikakati itakayosaidia makandarasi hao kutekeleza miradi mingi hasa ya kimkakati itakayoweza kuinua mitaji yao. “Linapokuja suala la ‘Local content’ yaani fursa za kiuchumi kwa watanzania, Mheshimiwa Rais kiu yake ni kuona ushiriki wa Makandarasi wazawa kwenye maendeleo ya Sekta ya Ujenzi unaongezeka”, amesema Bashungwa. Bashungwa ameeleza kuwa Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa idadi ya Makandarasi waliosajiliwa na Bodi ni 14,550 ambapo kati ya hao 550 ni Makandarasi wa nje na 14,000 ni Makandarasi wazawa lakini katika utekelezaji wa miradi Makandarasi Wazawa wanapata asilimia 46 na Makandarasi wa nje wanapata asilimia 54. Aidha, Bashungwa ameishukuru Serikali kupitia Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maboresho aliyoayaagiza katika sheria ya manunuzi kwa miradi yenye gharama ya kutoka Bilioni 10 hadi 50 kupewa kipaumbele kutekelezwa na makandarasi wazawa ili kuwajengea uwezo. Kuhusu madeni kwa Makandarasi, Waziri Bashungwa amesema kuwa kupitia Wizara ya Fedha, Serikali imeshaweka utaratibu wa kulipa madeni hayo ambapo hivi sasa kila mwezi kuanzia mwezi wa nane kiasi cha Bilioni 70 kinatengwa ambapo Bilioni 50 zinalipa madeni ya makandarasi wa ndani na Bilioni 20 ni kwa ajili ya kulipa Makandarasi wa nje. Bashungwa pia ameziagiza Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi kuhakikisha zinabuni mikakati ya kutangaza mafanikio na kazi zao kwa umma ili kuleta tija katika Taasisi hizo na Taifa kwa ujumla. Kadhalika, Bashungwa ameziagiza Taasisi hizo kusimamia wataalamu wao ili kuhakikisha wanatoa huduma sahihi na kwa wakati kwa umma na kuhakikisha wanachukua hatua kwa wale ambao watakiuka maadili ya kazi zao.
Photo by:Admin, 2023-09-27 08:34:12
photos are coming soon Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi. Godfrey Kasekenya amewataka Makandarasi wazawa wote nchini kuwa mabalozi wema kwa kufanya kazi nzuri zinzozingatia viwango na kukamilisha miradi kwa wakati ili Serikali ipate thamani ya fedha katika miradi yote. Agizo hilo amelitoa mkoani Mwanza akifungua mkutano wa kwanza wa Mashauriano wa Makandarasi na Wadau wa sekata ya ujenzi kwa Mwaka 2023 uliofanyika tarehe 30/03/2023 kikanda Mkoani Mwanza. “Ni muhimu kwenu Makandarasi kuzingatia uzalendo katika shughuli za kikandarasi pamoja na kutekeleza miradi kwa wakati na kwa viwango vyenye ubora kulingana na mikataba ili wanancho waweze kupata huduma bora kwa wakati na thamani ya fedha iliyokusudiwa” amesema Naibu Waziri huyo. Kasekenya amefafanua kuwa Makandarasi wana mchango mkubwa katika kuinua uchumi wa nchi yetu na endapo pale Makandarasi wanaposhindwa kutimiza wajibu wao wanawachelewesha wananchi kupata huduma zinazokuwa zimekusudiwa na pia wanaitia Serikali hasara.
Photo by:Admin, 2023-04-05 05:05:08
photos are coming soon Msajili wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) Mhandisi Rhoben Nkori ameishukuru serikali kwa kuendelea kutoa miradi mingi kwa wakandarasi wazawa ikiwemo ile ya ujenzi wa majengo ya utawala ya kiserikali, hospitali na barabara. Alisema hayo wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa Bodi ya mwaka 2022 kwa mgeni rasmi Naibu Waziri wa ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya pamoja na Makandarasi na Wadau wa Sekta ya Ujenzi katika ufunguzi mkutano wa kwanza wa Kikanda wa Mashauriano wa Makandarasi na Wadau wa Sekta ya Ujenzi unaofanyika jijini Mwanza tarehe 30/03/2023. Kauli mbiu ya mkutano huo ni " Kujenga Uwezo wa Makandarasi wa ndani: Mafanikio na Changamoto".
Photo by:Admin, 2023-04-05 05:04:40

Notice Board

Click "New" Icon Below To View Adverts

CONTRACTORS TRAINING COURSE ON CONTRACTS MANAGEMENT SKILLS-GOLD CREST HOTEL – MWANZA, OCTOBER 11 – 13, 2023
CONTRACTORS REVIEW INFORMATION FORM
EVENTS CALENDAR FOR THE FINANCIAL YEAR 2023/24
ORODHA YA MAKANDARASI WANAODAIWA (CONTRACTORS WITH OUTSTANDING FEES)
ONLINE PROJECT REGISTRATION MANUAL
PROCEDURE FOR CHANGING NAMES, SHAREHOLDERS AND DIRECTORS

Video Adverts

Photo Gallery

Subscribes For Newsletter