Tuesday 16th April 2024, 08:14 am

logo

The United Republic of Tanzania

CONTRACTORS REGISTRATION BOARD

  • crblogo

From The Press

photos are coming soon MAKANDARASI nchini wametakiwa kuzingatia mafunzo wanayopata kwa kuhakikisha wanayatumia kuboresha kazi zao wakati wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi. Hayo yamesewa Januari 29, 2022 mkoani Dodoma na Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi, Mhandisi Consolata Ngimbwa wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa Makandarasi wazawa. Amesema CRB imejitahidi kuandaa mafunzo mengi yakiwemo ya namna ya kuandaa mikataba, kujaza zabuni kielektroniki na namna ya kuwasilisha zabuni hivyo lazima makandarasi wayatumie kuongeza ubora wa kazi zao. “Kuna mtu anachangia mada kwenye mkutano lakini akitoka hapo getini yote aliyojifunza anayaacha hapo sasa naomba tuyaishi haya tunayojifunza kwasababu ni kwa faida yetu sisi wenyewe kukuza biashara hii. Mwezi ujao kutakuwa na mafunzo ya menejimenti na kufanya kazi kwa ubia naomba mhudhurie muongeze ujuzi,” amesema Amesema ni vizuri kuwatumia wataalamu kwenye utekelezaji wa shughuli zao lakini wanapaswa kutokuwa wategemezi kupita kiasi hivyo watumie mafunzo hayo kujiweka sawa na kuchana na utegemezi wa kujaza zabuni na kuendesha makampuni yao. Amesema kazi za ujenzi ziko nyingi lakini za ushindani badala ya kukaa na kulalamika kwamba hawapati kazi wayatumie mafunzo hayo kuongeza ujuzi hasa kwenye kujaza zabuni kielektroniki na kuweka bei ambayo ni halisia. “Hakuna kazi nyingi kwamba kila mtu atapata lakini zipo za ushindani na ili uweze kushindana kwenye soko hili ni lazima uwe na ujuzi mkubwa kwenye menejimenti, kujaza zabuni na kusimamia mikataba sasa ukisikia mafunzo njoo yana faida kubwa,” amesema Amesema Serikali imejitahidi kutangaza zabuni nyingi za miradi ya maji na ujenzi wa barabara hivyo makandarasi wa ndani wtakaobahatika kuipata wanapaswa kuitekeleza kwa ufanisi mkubwa. “Mkifanya vizuri mnajitengenezea njia yenu na ya wengine kuaminiwa ukifanya vibaya unatuharibia nasisi kuaminiwa. Biashara hii ya ukandarasi ni nzuri tu na ya heshima kwa hiyo hakikisheni mnalinda heshima ya kazi yetu kwa kufanyakazi nzuri,” amesema SOURCE: MICHUZI BLOGSPOT, 29 JAN 2022.
Photo by:Admin, 2022-02-02 08:30:51
photos are coming soon BODI ya Usajili wa Makandarasi (CRB), imewataka makandarasi kuacha woga kwenye kudai haki zao pale mikataba yao inapokiukwa kwa kuhofia kuharibu uhusiano na wateja wao. Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mhandisi Consolatha Ngimbwa, wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kuhusu usimamizi wa mikataba kwa Makandarasi wazalendo. Amewaasa watumie ujizi watakaoupata badala ya kuishia kwenye vitabu tu kwani uzoefu unaonyesha kwamba wapo Makandarasi ambao pamoja na kuwa na ujuzi, bado wanashindwa kusimamia haki zao eti kwa kuogopa kuharibu uhusiano na waajiri. “Msifanye hivyo kwa sababu katika mikataba Mkandarasi ana wajibu na haki zake na mwajiri vivyo hivyo. Hebu jiulize kwa nini Mkandarasi akikiuka makubaliano mwajiri hasiti kumchukulia hatua? Mbona Mwajiri haogopi kuharibu uhusiano,” amesema. Kadhalika, amewataka makandarasi wazalendo kutokurupuka wakati wa kusoma mikataba ya ujenzi ili kuepuka hasara wanayoweza kupata na wakati mwingine kukimbia kazi wanazopewa. Amesema usimamizi mzuri wa mikataba ni ujuzi wa muhimu na wa lazima kwa Makandarasi kwa sababu kimsingi kazi ya ukandarasi ni mikataba na kwamba nyakati zote, mkandarasi anashughulika na mikataba. SOURCE: MICHUZI BLOG 02/12/2021.
Photo by:Admin, 2022-01-01 08:30:51
photos are coming soon MAKANDARASI wametakiwa kuacha kuomba zabuni kwa gharama za chini, ili kuwavutia watoaji wa kazi, kwa kuwa uzoefu unaonyesha wamekuwa wakishindwa kuzikamilisha na wengine kukimbia baada ya kuzipata. Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Morogoro na Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Mhandisi Consolata Ngimbwa wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa makandarasi wazalendo. Alisema baadhi ya makandarasi wamekuwa wakijaza hela ndogo kama mbinu ya kushinda zabuni lakini wanapopata kazi hizo wanashindwa kuzikamilisha kwa wakati na wengine kushindwa kuzikamilisha kabisa. “Jazeni zabuni vizuri tena kwa uhalisia msijaze tu ilimpate zabuni lakini mwishowe zinawashinda, hapa katikati tuliyumba sana baada ya serikali kuanza kufanyakazi zake kwa kutumia utaratibu wa force account sasa tumeanza kupata kazi za serikali tusifanye makosa, tuzifanye kwa weledi mkubwa,” alisema Ngimbwa. Alisema CRB iliamua kuanza kutoa mafunzo hayo kwa makandarasi baada ya lawama nyingi kwamba makandarasi hao wamekuwa wakiweka bei ambazo hazina uhalisia. Mhandisi Ngimbwa aliwasisitiza pia kufanyakazi kwa ubia na makandarasi wenzao na wanaposhindwa kujua namna ya kuzifanya wafike ofisi za bodi hiyo au kwa wataalamu kwaajili ya kuelekezwa namna ya kufanyakazi za aina hiyo. “Wengi tunaingia kwenye kazi za ubia lakini tunashindwa sijui kwasababu hatuzijui au, uzuri wa kazi hizi ni kwamba mnaunganisha nguvu na kufikia vigezo vinavyohitajika na kama mkishindwa njooni CRB mtaelekezwa,” alisema. SOURCE: "Nipashe Alhamisi Agosti 12,2021"
Photo by:Admin, 2021-08-17 12:30:10

Notice Board

Click "New" Icon Below To View Adverts

Video Adverts

Photo Gallery

Subscribes For Newsletter